Jumapili, 31 Agosti 2014

VILE MUNGU ANAVYO KUJUA NI ZAIDI YA MWANADAMU ANAVYO KUJUA

VILE MUNGU ANAVYO KUJUA NI ZAIDI YA MWANADAMU ANAVYO KUJUA:
NI ZAIDI YA HATA SISI TUNAVYO JIJUA:
NI ZAIDI YA WEWE UNAVYO JIJUA MWENYEWE:



Kibari chako kiko katika mema unayo yafanya siku zote
haswa  katika kazi ya MUNGU
MUNGU anafahamu makusudio ya mwanadamu kabla ajafika katika jambo ambalo wenda angelifanya wiki,mwezi,au hata mwaka unaokuja
MUNGU aliona kusudio la kaini alipo taka kumuangamiza nduguye Habili,akamwambia  kuna dhambi ina kutamani hapo baadae
MWA4:6-8
BWANA akamwambia kaini ,kwanini una ghadhabu? na kwanini uso wako umekunjamana?kama ukitenda vyema utapata kibari?Usipo tenda vyema dhambi iko,inakuotea mlangoni,nayo inakutamani wewe,walakini yapasa uishinde.
Ni kwamba MUNGU aliona kilicho kuwa mbele ya kaini akamwambia inapasa uishinde,tabu juu yetu hatuifahamu sauti ya MUNGU,na kama tunaifahamu tunafanya ugumu wa mioyo

Nitakuambia MUNGU anapateje kujua na kuona sili zako ambazo hata wewe haujui nini kitatokea hapo baadae
Alikuwepo nabii mmoja ,baada ya MUNGU kuiona safari yake kuwa si salama alimwambia usile,usinywe,wala usirudie njia uliyo itokea maana MUNGU aliona, nini kitakacho mpata iwapo ata kwenda kinyume na maagizo hayo, yeye mwenyewe hakufahamu lo lote hata alipodanganywa alikubali.
1FALM 13:16-17
Nae akamwambia,siwezi kurudi pamoja na wewe,wal kuingia pamoja na wewe;wala sili chakula,wala sinywi maji pamoja nawe hapa, kwani nimeambiwa,kwa neno la BWANA,
Usile chakula ,wala usinywe maji huko,wala usirudie kwa njia ile ulioijia

MUNGU alifahamu Mtu huyu asipoenda hivyi atapatwa na madhara makubwa aidha mauti
Msikilize MUNGU ndiye aliye na njia zako bila MUNGU hakuna kitu ni kama gari bila dereva gizani
Hata YESU alipo waagiza petro na yohana,kuandaa pasaka walishindwa ,wtaandaa wapi,ikabidi waulize  ndipo akawaambia
LK 22:9-10
Wakamwambia wataka tuandae wapi?Akawaambia tazama, mtakapoingia mjini mtakutana na mwanamume akichukuwa mtungi wa maji, mfuateni mkaingie katikanyumba atakayoingia yeye
walikuwa hawafahamu lolote ,lakini kwa yesu picha na umbo la hiyo pasaka lilikuwa moyoni,si kwamba labda aliwahi kwenda na kufanya mawasiliano au kumuomba yule mwenye mtungi, hapana yeye kwa uwezo wake alifahamu
mifano hii najaribu kukuonyesha kuwa MUNGU anaona na kufahamu kabla yako wewe hujafahamo lolote
Pia kama vile MUNGU alivyo fahamu mawazo ya Kaini vivyo hivyo alifahamu mawazo ya Yusufu juu ya mke wake Mariamu alipo kusudia kumuacha,pia mwana mke msamari aliyekutana naye kisimani
YN 4:15
Yule mwanamke akamwambia BWANA unipe hayo maji nisione kiu wala nisije hapa kuteka, YESU akamwambia nenda kamwite mumeo uje naye hapa.Yule mwanamke akajibu akasema sina mume
{YESU akamwambia umesem vyema sina mume .Kwamaana umekuwa na waume watano naye uliye naye sasa siye mume wako,hapo umesema kweli}
MUNGU anafahamu kusudi lako,PETRO alijiona kwakuwa yuko na yesu na watu walivyo msifia kuwa ,unafanana na YESU alijenga kiburi na kuona kila jambo anaweza YESU akamwambia PETRO wewe utanikana maratatu kabla jogoo ajawika,maana aliangalia kwa uzoefu wake akaona imani ya PETRO bado,kwahiyo tunapo patwa na hali ngumu huwa tuna mkana YESUna YESU anajua kabisa kuwa utamkana
nimalize mpendwa wangu kwa kukupa sababu za MUNGU anapateje kujua mambo juu yako unayo yawaza na yatakayo kutokea baadae au siku za usoni,kamavile MUNGU alivyo ona hatari iliyo taka kumpta mkulima,aliyesema Ee nafsi yangu tulia sasa ule na kunywa MUNGU akamtokea akamwambia, mpumbavu wewe leo wanitaka roho yako,Hicho ulichojiwekea hakiba kitakuwa cha nani?niache huko maana si lengo tika lengo;
MIT 20:27
Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleka yote yaliyo ndani yake
Kwahiyo mpendwa wangu ,yote yote utakayo waza ujawaza umeona ujaona taalifa yake inaenda,tena unaipeleka mwenyewe,je ni nini utakacho kifanya asijue MUNGU? au katika mabaya utajificha wapi usionekane na bwana?kwakuwa MUNGU wetu ana tupenda ,anapoona jambo la hatali katika taalifa yako,anakuhimiza omba kama umeokoka na mana ujaokoka anakuhimiza okoka,
yeye husema na kila mmoja awe ameokoka au ajaokoka.labda pumnzi yako ikome au usiitumie pumzi ya mungu,kama itawezekana,na ninajua ni ndoto,kwahiyo ili uishi salama wewe ambaye umeokoka ni kujaza maneno ya MUNGU moyoni ili ikienda taalifa iendea yenye utukufu
Nawewe ambaye bado ujaokoka sikutishi bali ninakuomba uchukuwe hatua ya karibu na umpokee YESU ili ukurasa wako ubadilishwe na inapokwenda taalifa iwe ni utukufu
usijidanganye,hatakama ujaokoka taalifa inaenda aiajalishi uko katika hali gani
MUNGU AKUBARIKI SANA NA UZIDI KUSONGA MBELE


Mwinjilisti JOHANNES R MNIKO
0712  565 676                                   Askofu doct BARNABAS I KIMBE
    PGMM                                                       0653 395 344/0754 395 344
VINGUNGUTI                                                    PGMM
DSM                                                                  VINGUNGUTI 
                                    KARIBUNI
Najua wengi mnamzigo wa kuwaeleza watu wa MUNGU maneno ya uponyaji basi tuwasiliane ili utumie blogg hii kwa kukiokoa kizazi hiki ambacho shetani anajisifu kuwa amekimiliki,tumika ili watu wa MUNGU wapone,pia kama tuko pamoja LIKE 

Jumapili, 24 Agosti 2014

BARAKA ZAKO ZIPO KAA MKAO WA KUPOKEA

BARAKA ZA MUNGU  UENDANA NA UNYENYEKEVU
UTIIFU WA NENO LA MUNGU ;
NA KULIISHI NENO LA MUNGU


HALOO
mpendwa wandu leo nakuja na ujumbe wa bwana  kwa ajili ya maisha yetu ya kila siku
haswa hususani katika kuhitaji baraka za MUNGU ,
KWA NZA NIKUSALIMU KWA JINA LA YESU KRISTO MWANA WA MUNGU ALIYE JUU;

Watu wengi sikuizi wanaomba baraka kwa MUNGU na wengine hata kuhama makanisa kwa kuhitaji tu eti abarikiwe
zipo kanuni za MUNGU na miungu pia
MUNGU anataka utende mema tu
miungu inataka utende dhambi tu
sasa bas kwakuwa miungu inaishi dhambini itapenda uifurahishe katika dhambi;
MUNGU wetu anaishi katika haki ,anapenda utende haki ili uweze kubarikiwa;
MUNGU anasema na sisi kila iitwapo leo kuhusu haki yetu ya baraka,ambazo ziko sipesho juu ya wale woote anao wapenda;
ndiyo maana anajalibu kutuweka sawa iili tufikie kiwango cha kuiachilia baraka kwetu

ISAYA 1:15-19
Nanyi mkunjuapo mikono yenu,nitaficha macho yangu nisiowaone;naam,muombapo maombi mengi,sitasikia;mikono yenu imejaa damu,16 Jiosheni, jitakaseni,ondoweni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu acheni kutenda mabaya; 17 jifunzeni kutenda mema;takeni hukumu na haki; wasaidieni walio onewa ; mpatieni yatima haki yake;mteteeni mjane.

ukiisha yafanya haya  yote yalyo andikwa hapo juu ,MUNGU  anasema
18 haya njooni tusemezane asema BWANA dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana,zitakuwa nyeupe kama theruji;zijapo kuwa nyekundu kama bendela,zitakuwa  kama sufi19 kama mkikubari na kutii, mtakula mema ya nchi
kumbe mpendwa wangu ni uamuzi wako kukubari au kukataa,MUNGU atulazimishi kuzipokea baraka
ni wewe
uwe na sababu ya taharuki,jibu sio kuhama kanisa ,omboleza umuambie MUNGU  hapa sitoki adi umenijibu;omboleza hapo hapo ulipo
YER 14:2
Yuda huomboleza, na malango yake yamelegea;wameketi chini wamevaa kaniki;na kilio cha yerusalemu kimesikika juu
kuna jambo unalo weza kulifanya mbalo lita mgusa BWANA moja kwa moja,ebu lejea hapo juu katika isaya  ususani mstari wa 17 hapo utakuwa umekubariwa na MUNGU  na umemgusa
hata kama utahama kanisa bila kufuata kanuni za MUNGU,hatauendako hakuna lo lote
MIK 3:4
Ndipo watakapo muita BWANA, asiwaitikie;naam,atawaficha uso wake wakati huo,kwa kadri walivyo tenda mabaya kwa matendo yao.
jitambue kuwa sasni wa MUNGU na nilazima ulidhi yote kutoka kwa BWANA hakuna kupokea kama uko mguu mmoja duniani na mmoja kwa yesu;utashanga wenzako wanabarikiwa na wewe ubarikiwi, wewe ujajua sili ,sili ni kusikia na kutii basi
YAK 4:3
Hata mwaomba ,wala hampati kwasababu mwaomba vibaya,ili mvitumie kwa tamaa zenu
ni lazima tudumu katika mapenzi ya BWANA ndipo BWANA atakapodumu katika mapenzi yetu
MUNGU wa Isaka Ibrahimu  na Yakobo akusaidie ili kufikia malengo yako siku zote



mwinjilisti Johannes R Mnico
vingunguti sheli
PGMM church
0712 565 676
                                                                Askofu Doct Barnabas I Kimbe
                                                                    PGM missioni
                               KARIBU SANA HUDUMA ZIPO

Jumapili, 10 Agosti 2014

VITA NI VYA BWANA ,USIPATE SHIDA

                                VITA NI VYA BWANA:                       BWANA YEYE HAOKOI KWA UPANGA

IPO SIRAHA JUU YU MTU WA MUNGU,INAYO MLINDA NA KILA JAMBO BAYA,AMBALO SHETANI ALIKUSUDIA KWA MTU WA MUNGU;




Kila siku huwa kunajambo ambalo mtu wa MUNGU anapitia  iwe baya au zuri
lakini haitufanyi sisi kushindwa kusonga mbele na wokovu
Ni kweli yapo majaribu ambayo  katika macho haya  inakuwa huwezi kusimama mbele yake
NI kama vile macho ya wana wa ISRAEL yalivyo muona Goriati kuwa ni mtu asiye weza kupigwa na ni mtu wa kuhofiwa sana
Lakini.nikwa sababu wengi hawajui uwezo wa NENO Nikama nilivyo ongelea uwezo wa NENO na kumkaribia MUNGU, nilizungumza katika chapisho li lilo pita
na hapa vile vile tunaona uwezo wa NENO DAUDI Alitumia NENO kumuua Goriati
YEREMIA aliambiwa niite nami nitakuitika na nitakuonyesha mambo magumu na magumu ambayo sisi hatukufikili,ni kwanini? ni kwa kulisoma NENO1.SAMWEL 17:42-47Hate wafilisti walipotazama huku na huku,akamwona DAUD Akamdhalau ; kwa kuwa ni kijana tu,tena anasura nzuri.Mfulisti akamwambia DAUD ,je! mimi ni mbwa hata unijie kwa  fimbo?Mfilisti akamlani DAUD Kwa miungu yake.Mfilisti akamwambia DAUDI njoo hukuNdipo DAUDI  akamwambia yule mfilisti ,Wewe unanijia mimi kwa upanga na fumo na mkuki, bali mimi nakujia kwa jina la BWANA wa majeshi MUNGU wa majeshi ya Israel uliyo watukanasiku hii ya leo BWANA atakutia mkononi mwangu,nami nita kupiga,na kukuondolea kichwa chako nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya wafilisti ili kwamba dunia nzima ijuwe yakuwa yuko MUNGU katika Israel nao jamii ya watu wote pia wajue yakuwa BWANA HAOKOI KWA UPANGA WALA KWA MKUKI;MAANA VITA NI VYA BWANA  NAYE ATAWATIA NINYI MIKONONI MWETUje  wewe leo unasema neno gani kwa Goriati wako?maana tunajua kila mtu anaye Goriati wake
iwe kwenye ndoa,
familia yako
kazini kwako
maisha yako ya kila siku
je ? unamtamkia nini ?au kulingana na ukuwa wake unabaki una ugulia?sema NENO juu ya Goriati
wako mwambie hutoonekana tena milele
Mpendwa,jaribu lina masikio linasikia  kataa udhaifu
DAUD hakukili udogo wala kushindwa alimwamini MUNGU wa baba zake
MUNGU AKUBARIKI  SANA MPENDWA WANGU  ususani wewe mdau wa usawa wa neno bloggsport                                                     KARIBU IBADAN I:Mwinjilist Johannes R Mnico0712565676PGMMVINGUNGUTI DSM                                                             Askof/Doct BARNABAS I KIMBE                                                                           PGMMchurch                                                              0754395344-0653395344                                                                  VINGUNGUTI                        

Ijumaa, 8 Agosti 2014

NENO LINAUMBA,NENO LINA PONYA, NENO LINA BARIKI

KULISOMA NENO,KULIFAHAMU NENO,KULIKABILI NENO,NA KULIISHI NENO
KULISOMA NENO NI KUMSOMA MUNGU,KULIFAHAMU NENO NI KUMFAHAMU, MUNGU
KULIKABILI NENO NI KUMKABILI MUNGU,NA KULIISHI NENO NI KUMUISHI MUNGU

KUSOMA NENO;
MKIRISTO imempasa kusoma neno maan ndiyo sehemu pekee ya kumjua MUNGU  na kujua nini MUNGU ana taka kusena na wewe kwenye kusoma neno utajua nini baya na nini zuri ambal MUNG anapenda kwako lifanyike,kuna maneno ya kutiwa moyo wakati wa majaribu,na uliona jaribu lilo kubwa ulione dogo ni kwakuwa umesoma neno,jaribu halitakuondoa kwenye msingi ulio ujenga kwenye neno maana utakuwa mikononi mwa MUNGU si ndiye neno,,,!
YN 1:1
Hapo mwanzo kulikuwepo na NENO, naye NENO alikuwepo kwa MUNGU,naye NENO alikuwa ni MUNGU.
Kwahiyo tunaona yeye ndiye NENO Pia biblia yangu inaniambia kuwa yeye ndiye MWANZO
2-3 huyo WANZO alikuwako kwa MUNGU  vyote vilifanyika kwa huyo;wala bila yeye hakikufanyika chochote  kilicho fanyika 
tunayafahamu haya yote kwa kusoma NENO
Pia kuna kuonywa katika NENO; Maana biblia ina sema ipo njia ionekanayo machoni pa mtu kuwa ni salama kumbe ni njia iendayo upotevuni;
kwahiyo neno pekee ndiyo inaweza kukuonyesha njia zako kuwa ni salama au si salama na kukuonya
kwahiyo tunayo sababu kuyafahamu maonyo na kumtukuza MUNGU
1 EBR 1:10
Na tena, Wewe,BWANA,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi,na mbingu ni kazi za mikono yako 
tuna mtukuza MUNGU kwakuwa tumemfahamu kwa NENO, Unapo lijua NENO umemfahamu MUNGU
Tunapo kuwa hatujali pale ambayo MUNGU anasema ni kwa sababu hatusomi NENO
Kuna kuisikiliza sauti ya MUNGU pale unaposoma NENO usilione NENO kuwa ni kitu cha kawaida MUNGU azoeleki hata siku moja  isiwe ni mazoea kuitwa wewe mlokole au mkiristo
hiyo inamchukiza sana MUNGU
AYUB 38:4
Ulikuwa wapi nilipo iweka misingi ya nchi? Haya!sema, kama ulikuwa na ufahamu
Ninani aliye amrisha vipimo  vyake,kama ukijua ?
au ninani aliye nyoosha kamba juu yake?
mimi na wewe hatujui lakini tunapolisoma NENO ROHO wa MUNGU ana tushudia na kutufundisha haya yote,ISIFIKIE WAKAI ADI mungu ANA TURUDI KWA BAKOLA KWAKUWA HATUSOMI NENO
hii ninaifananisha na wana wawili ambao mmoja alipenda kuketi miguuni pa baba yake akijifunza  na kula pamoja na baba yake
na wa pili yeye alipenda michezo hakujari kuwepo nyumbani ikafikia hata kuweka uadui na baba yake
alipata faida gani
kunacho weza kutuokoa ni NENO  maana biblia yangu inaniambia;nimeliuma NENO langu kuwaponya na kuwaokowa kwenye maangamizo
pasipo NENO kuna kuangamia,kwenye NENO kuna kuponywa kainahaja kuwasumbua watumishi wa MUNGU mimi nilipofahamu uponyaji uko wapi niliacha kuwasumbua watumishi wa MUNGU
ISA 44:24
Tena YEREMIA akawaambia watu wote,na wanawake wote,Lisikilizeni NENO hili la BWANA,ninyi nyote wa Yuda,mliopo hapa katika nchi ya misri
tangu kale NENO  lilikuwa ni muhimu hapa hakuna shotikati
NENO hufanya imani hata kufanya mtu kuamini na kutenda jambo furani
RUM 1:20
Kwa sababu mambo yake yasiyo onekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana,na kufahamika kwa kazi zake, yaani,uweza wake wa milele na UUNGU wake;hata wasiwe na udhuru ni kwa sababu ya NENO la MUNGU  ni kwa uweza wa NENO la UUNGU
NENO linaumba kama nilivyo ongea hapo nyuma  lina ponya
KOL1:16
Kwakuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa,vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi,vinavyo onekana na visivyoonekana,vikiwa ni viti vya enzi ,au usurutani ,au enzi, au isultani,au enzi,au mamlaka vitu vyote vimeumbwa kwa ajili yake,na kwa ajili yake.
yote haya tunayafahamu kwakuwa tunasoma NENO
ROHO mtakatifu anaishi katika NENO hicho ndicho chakulla cha ROHO mtakatifu
UFU4:11
MUNGU AKUBARIKI SANA upate kujua NENO kulitumika




Mwinjilisti  Johannes Range
0712565676
PGMM church
                                                          Askofu/ Dct BARNABAS E KIMBE
                                                                 PGMM Church
                                                            0653395344/0754395344
KARIBU HUDUMA ZINAENDELEA KILA SIKU
Usikose kuuliza juu ya lile linalo kukwaza utajubiwa na kusaidiwa
            KARIBU MUNGU akubariki mpendwa wangu ususani wewe mdau wa blogg yetu ya USAWA WA NENO

Jumapili, 3 Agosti 2014

ULICHO NACHO NDIYO MTAJI USIPUUZE.

                                               NIKUFANYIE NINI?
                               NIAMBIE UNANINI NYUMBANI KWAKO?


HALLOW WAPENDWA WANGU WA usawa wa neno blogsport mnaopenda kujifunza maneno ya MUNGU  kupitia blog yako
Leo tuakumbushana kuhusu uweza,nguvu, na uweza wa YESU KRISTO
NENO HILI AMELIFUNDISHA VIZURI SANA askofu Barnabas Emanuel Kimbe wa kanisa la PGM Church vingunguti

 NIKUPE TU SEHEMU YA MAHUBILI YAKE NILIYO KUTUNZIA WEWE  MPENDWA WANGU wa usawa wa neno blogsport

2falme 4:1-7

Basi mwana mke mmoja miongoni mwa wake wa wana wa manabii alimwendea Elisha,akasema, mtumishi wako mume wangu amekufa;nawe wajua kwamba mtumishu wako alikuwa mcha BWANA na aliye mwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa .................................!!! soma adi mstari wa 7
ujumbe: 
wapendw hatujazuiliwa kukopa,isipokuwa tulipe madeni  ya wale waliyo tuamini na kutukopesha,
biblia inasema asiye haki ukopo asirudishe ,aliye hahi ukopa na akarudisha
lakini tukumbuke madeni ya zamani ni tofauti na ya leo hii ,zamani ulikuwa ukikopa na ukashindwa kulipa,ulikuwa unapelekwa mnadani unauzwa lakini leo ipo neema
Yule mama alipo ambiwa na Elisha alitii kumbe pia kuna kutii
Tulia kwa YESU tii kiapo chako cha kwanza, unababaika nini  tulia
Yule mama jinsi walivyo  mfikilia ilikuwa sivyo
hata wewe leo wanekupajuna,lakini lipo jina alilo kuandalia BWANA
mtu yeyote anapo inuliwa huwa na jeuli na imani inakuwa zaaidi
Kunafaida kubwa ktika kumtegemea YESU,kuaibika kwako ni kwa mda tu,japo kunamateso lakini hautadumu maana neno linasema mateso ya mwenye haki ni mengi mno, 
Lakini bwana umponya nayo yote
siku hizi za mwisho wengi wamechanganyikiwa hawajui nini la kufanya
msaada ni kwa YESU peke yake ,hakuna kitu nje ya YESU
kwakuwa shetani anajua nini uhitaju wako basi basi anaiyubisha imani yako tulia uliko achana na imani za dini
Leo mtu akiona afanikiwi anakimbia kanisa huku nahuku
imani ni kuwa na hakika ya mambo yatalajiwayo,
ni bayana ya mambo yasiyo onekana kwa macho
LEO MPENDWA ANA TAKA ASHIKE APAPASE WAPI NAWAP?
unapotaka kujibiwa haraka shetani nae anatengeneza ant fisho ukiona unasema eeee huu ndio muujiza wangu ,kumbe ni mtego wa kukuangamiza
cheki mfano huu fimbo ya MUSA ilipo geuka nyoka farao naye alifanya muujiza kama huo huo tofauti nyoka wa MUSA alikuwa ni originar akameza wale ant fisho wa farao
kwahiyo shetani anauwezo wa kutengeneza muujiza  tulia kwa YESU


mWINJILIST johannes R Mnico
0712565676
vingunguti
PGMM church
                                                     Askofu mkuu  Dct BARNABAS I KIMBE
                                                        0653 395 344/0754 395 344
                                                        PGMM Church
                                                         vingunguti sher
KARIBUNI WOTE HUDUMA NA IBADA ZIPO KAMA KAWAIDA
MUNGU awabariki

Jumanne, 29 Julai 2014

NEEMA YA MUNGU NA HURUMA ZAKE KWETU

TANGU ADAMU WA KWANZA HATA ADAMU WA SASA :
WAMEJENGWA NA KUTO JARI;HATA KUYAPUUZA MAAGIZO,AMRI NA MASHAULI:



           Nikweli kuwa kibuli na dhalau pamoja na kutojali kunafanya binadamu kujengeka na kiburi
mfano: kutojari mtuanapoambiwa jambo anasema nita tenda,afu anakamatwa na uvivu furani na                        anajikuta hajatenda
           sio yeye ni vile amekubari afu hajachukuwa hatua, na shetani hutumia nafasi hiyohiyo                          kuwakosanisha
             
mfano: MUNGU alipomwambia ADAMU mitiyoote matunda yake waweza kula lakini huu tuu usile                    hakika siku utakayo kula utakufa,
           shetani alipo isikia ile HAKIKA akaifanyia kazi
MUNGU anaposema jambo huwa amelidhibitisha ni kweli halitokengeuka wala kubadilika
 Angalia HAKIKA aliyosimamia:
MWA 3:5
       Kwamaana MUNGU anajua ya kwamba siku ile mtakayo kula matunda ya mti huo,mtafungliwa macho,nanyi mtakuwa kama MUNGU,mkijua mema na mabaya.
hii ndiyo HAKIKA aliyosimamia shetani


EBU jiulize shetani baada ya kutenda dhambi pamoja na ADAMU wa kale, hadi leo anatumikia hadhbu aliyo adhibiwa, anakwenda kwa tumbo,anakula mavumbi pia
Lakini mwanadamu anataka kulahisisha hadhabu ya MUNGU

mfano
         mwanaume aliambiwa atakula kwa jasho lakini kwa mwanaume inakuwa ni ngumu
yeye anataka apate vya lahisi lahisi visivyo mtoa jasho sawa, anafanikiwa lakini baraka za MUNGU hazipo hapo wala mkono wa MUNGU haupo hapo mwanzo 3:17

mwanamke yeye aliambiwa utazaa kwa uchungu,lakini leo wanamama wengi wanapo taka kujifungua anaenda kwa waganga ili ajifungue salaama wengine hudiliki kwenda kwao katika mizimu kuiomba imsaidie aliisha sahau kuwa kuzaa kwa uchungu ni agizo la MUNGU

Jambo lingine ni vyakula hapo sasa ndipo tumekengeuka kabisa
MWA 3:17
               Akamwambia adamu,kwakuwa umeisikiliza sauti ya mke wako,ukala matunda ya mti ambao nilikuagiza,nikisema Usile:ardhi imelaaniwa kwa ajili yako:kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako ;michongoma na miiba itakuzalia,nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula,hata utakapo irudia ardhi,ambayo katika hiyo ulitwaliwa;kwa maana u mavumbi wewe,,nawemavumbini utakwenda

hili ni agizo kijana wa leo wao ni kijiweni halijui agizo, lakini pamoja na agizo hili mwanadamo wa leo kaachia nafasi na shetani akaitumia nafasi hiyo pamoja na mawazo yetu na tunakuta tuna fanya jambo sikuzote halimpi MUNGU utukufu

jambo lingine ni mitandao ya kijamii ivi kweli kama kweli kwa haya yanayo fanyika leo MUNGU je ana tufikiliaje? je? hilo ndilo agizo,tusidanganyike na neema iliyoko mbele yetu

hakuna kujificha kwa matendo yako,kuna wengi wanasema nimeokoka nampenda YESU lakini haendani na maneno hayo ,nataka nikuambie rafiki yangu utamficha mwanadamu lakini kwa MINGU uko uchi afadhari na ulipo zaliwa ulisitiliwa,kwa MUNGU uko uchi
 MITHARI 20:27
                    Pumzi ya mwanadamu ni  taa ya BWANA,
                     Hupeleka yote yaliyomo ndani yake
Lolote unalo waza ndg yangu,taarifa inaenda
liwa jema au baya hakuna siri kwa MUNGU  
MUNGU wangu wa mbinguni na akubariki sana 

Mwinjilist  Johannes R Mnico
0712565676
PGMM church
VINGUNGUTI 
D,Salaam 
                                                           Askof, BARNABAS I KIMBE
                                                                     0754395344/0653395344
                                                                      PGMM Chur chu 
                                                       PENTEKOST GOSPEL MISSION &MINISTERS

Ijumaa, 25 Julai 2014

MBASHA NA FLORA WAPATANA NA KUISHI PAMOJA TENA


MBASHA, FLORA WAPATANA


Ule mtafaruku ndani ya ndoa ya mwimba Injili mahiri Bongo, Flora na mumewe, Emmanuel Mbasha umedaiwa kumalizika kwa wawili hao kupatana, Risasi Jumamosi linakuwa nambari wani kukuhabarisha.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, wawili hao walikalishwa kikao cha upatanishi mapema wiki hii kilichokuwa chini ya familia.
Mume wa Flora Mbasha, Bw. Emmanuel Mbasha.
MANENO YA CHANZO
“Kikao cha familia kilikaa, Mbasha aliitwa akafika, Flora naye aliitwa akatokea, mazungumzo yalikuwa marefu lakini kimsingi waliamua kuweka kando mtafaruku wao na kuijenga upya ndoa yao,” kilisema chanzo.
Chanzo kiliongeza kuwa katika kikao hicho cha mwanzoni mwa wiki hii, miongoni mwa adidu za rejea ilikuwa kutokumbushia vikao vilivyopita ambapo hakukupatikana muafaka.
VIKAO VILIVYOPITA
Katika vikao vilivyopita, wahusika wakuu walikuwa wazazi wa Mbasha (mzee Maneno Mbasha, Zulfa Maneno), ndugu wa Flora na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
Mwimbaji Injili mahiri Bongo, Flora Mbasha.
VIKAO VYA BAADAYE
Kwa mujibu wa chanzo, vikao vilivyofuata, wawili hao wakawa tayari kila mmoja ametema nyongo yake pembeni na kufikia makubaliano kwamba, ndoa yao isimame tena wakitumia maandiko kwenye Biblia kutoka kitabu cha Waebrania yanayosema:    Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
WAKORINTHO YAFUNGA KAZI
Kwa mujibu wa chanzo hicho, maneno mengine ya Biblia yaliyotumika kwenye kikao hicho mpaka wawili hao wakaamua kurudiana ni 1 Wakorintho 7:1-10 ambapo maandiko yanasema:
Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
Flora Mbasha akiwa kwenye picha ya pamoja na mumewe, Emmanuel Mbasha.
Mke hana amri juu ya mwili wake bali mumewe vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake bali mkewe. Msinyimane, isipokuwa mmepatana kwa muda ili mpate faragha kwa kusali, mkajiane tena shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza, wala hapo si mimi, ila Bwana (Mungu), mke asiachane na mumewe, lakini ikiwa ameachana naye na akae asiolewe au apatane na mumewe, tena mume asimwache mkewe.
KIKAO CHA JUMAMOSI KUMALIZIA
Chanzo kilisema kuwa, kikao cha mwisho ambacho kitamalizia kuweka mambo sawa ili wawili hao waanze ngwe ya pili ya ndoa yao ambayo inaaminika itakuwa ya mwisho mpaka kifo kiwatenganishe, kinatarajiwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam mahali ambapo hapakutajwa.
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
MWANASHERIA ATAJWA
Mwanasheria wa Flora aliyejulikana kwa jina moja la Ado ametajwa kusimamia kikao hicho ili wawili hao waanze maisha mapya baada ya safari fupi ya mvurugano uliowafanya kuwa mbalimbali.
AONGEA NA RISASI JUMAMOSI
Juzi, Risasi Jumamosi lilimsaka mwanasheria huyo kwa njia ya simu yake ya mkononi ili kumsikia anasemaje kuhusu kutajwa kwenye usuluhishi wa ndoa hiyo ambapo alipopatikana alisema:
“Niko Arusha, Ijumaa nitarudi Dar. Kuhusu kikao cha usuluhishi siwezi kukwambia lakini suala la kuwapatanisha nalifahamu, nawaomba na ninyi msaidie kufanikisha jambo hilo zuri.”
VIPI KUHUSU KESI YA MADAI YA KUBAKA?
Hata hivyo, Wakili Ado hakutaka kugusia kuhusu kesi ya Mbasha iliyopo Mahakama ya Wilaya ya Ilala ambapo anadaiwa kumbaka shemejiye mara mbili (jina tunalo) ambayo kwa mujibu wa mahakama, upelelezi umekamilika na itasikilizwa Julai 17, mwaka huu.
KWA UPANDE WAKE FLORA
Risasi Jumamosi lilimwendea hewani, Flora ili kumsikia anasemaje kuhusu kuwepo kwa upatanishi kati yake na mumewe, Emmanuel.
Huyu hapa: “Ongea na wakili wangu atakwambia kila kitu.” Ambapo majibu ya wakili yalikuwa: ”Ninachojua mimi ni kwamba Flora ameshamsamehe mumewe na yuko tayari kuanza ukurasa mpya.”
MBASHA SASA
Kwa upande wake, Mbasha alipozungumza na gazeti hili juzi alisema kurejea upya kwa ndoa yake ni jambo la kuupendeza moyo wake.
“Mimi sina neno nipo tayari, nimeshasamehe yaliyotokea, Flora ni mke wangu jamani, nampenda sana kutoka moyoni.”