Alhamisi, 24 Julai 2014

IMANI NI SEHEMU AMBAYO WAKRISTO TUMEIPOTEZA:

WAKRISTO TUMEPOTEZA SEHEMU MUHIMU SANA
AMBAYO HATUWEZI KUFIKIA VITU VYA ROHONI PASIPO HIYO IMANI: 

Watanzania wenzangu, ususani wakristo kuna jambo ambalo linalo achiliwa furaha na MUNGU wetu kuja kwetu kama unaishi na IMANI na sio kuwa na IMANI maana YESU alisema ,ukiwa na IMANI kama punje ya haradani unaweza kuuambia mlima huu ng'oka nao ukatii VITUVYOTE BILA IMANI HAIWEZEKANI unapokuwa na imani unampendeza MUNGU kuna vitu ambavyo MUNGU ameahidi ambavyo tunavipokea kwa imani

ukisoma kumbu kumbu la torati 28 kunavitu vingi ambavyo utekelezaji wake ni IMANI je? unajuwa ni kwanini IBRAHIMU aliupendeza moyo wa MUNGU ? ni kwa sababu alikuwa na imani na alimwamini saana MUNGU na ndo maana alipata hata nafasi ya kuitwa rafiki wa MUNGU

LUKA mwanafunzi wa YESU, baada ya kuijua imani alidiliki kuandika yale ambayo YESU alisema mwenyewe
LK 21:15
              Kwasababu mimi nitawapa kinywa na hekima ,ambayo watesi wenu wote  hawata weza kushindana nayo wala kuipinga 

lakini sasa huwezi kupokea siraha hii kubwa pasipo kuwa na IMANI maana hivi vyote umekwisha kupewa lakini hatuja pokea  kwa kuwa hatuna IMANI
Mwenye IMANI  anafundishika,hata MUNGU uingilia kati juu ya mafundisho yake,mpenda ni MUNGU anaye achilia vyote kukufuata ;afuataye baraka hana imani, aliye na imani atavumilia kila hali,akimtumai MUNGU
YESU alisema na wote watakuwa wamefundishwa na MUNGU Ili kuishikilia IMANI yao
YN 6:45 
             Imeandikwa katika manabii, na wote watakuwa wamefundishwa na MUNGU,basi kila aliyesikia na kujifuza kwa BABA Huja kwangu,

kwahiyo imani inajengeka kabla ya kumjua YESU na unapo  okoka ndipo unazidi kukua ki IMANI,
Lakini pia leo tunaye ROHO mtakatifu ndiye anayefanya kazi ya kutupandikizia IMANI
IMANI inazaa vitu vingi sana,

mfano :hekima,maalifa,uaminifu,upendo, utu wema,kujari,na vingine vingi
YAKOBO asema ukipungukiwaq na hekima uombe dua lakini dua yenyewe ni lazima uwe na IMANI Maana maandiko yanasema kila amwendeaye MUNGU ni lazima aamini yupo kwahiyo lazima uamini

YAKO 1:5  
                 Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa MUNGU awapae wote kwa ukalimu, wala hakemei;naye atapewa 
Utapewa kama utakuwa na imani na kuamini juu ya lile uombalo,usijaribu, IMANI haijaribiwi
BWANA YESU asifiweeeeeeeeeee,,! Haleluyaaaaaaaaaa,,!
amina na MUNGU akuhifadhi na kukutetea  mpendwa wangu
tuombe,,,! 
                             BABA katika jina la YESU KRIST O 
                              ninamuweka msomaji wa nakala hii 
                              mikononi mwako ukamjaze imani 
                              ya kweli na tumaini la mbinguni  
                               ukamkumbuke pia katika uzima 
                                  wa milele na haja ya moyo wake ukampe 
                            ni katika jina la YESU  KRISTO 
                                    nimeomba na kuamini 
                                          Imeen...!
mwinjilisti Johannes R mnico
0712565676 
PGM CHURCH 
VINGINGITI 
                                Askofu, BARNABAS, I ,KIMBE
                                 0754395344 / 0653395344
                             KARIBU  PENTEKOST GOSPEL MISSION
                                  Huduma zote za ki ROHO zinapatikana

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni