Jumapili, 13 Julai 2014

KWA TAARIFA YAKO: NAMNA WAISLAMU, WAKRISTO NA WAYAHUDI WANAVYOTAKA KUABUDU PAMOJA

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu

KWA TAARIFA YAKO unaweza kuwa unafahamu historia ya ule ukuta wa berlin ulivyowagawa Wajerumani mnamo miaka ya 60, lakini hujajua ni namna gani taifa hilo liko kwenye mchakato wa kujenga nyumba moja ya ibada kwa waislamu, wayahudi na wakristo kwa wakati mmoja, yaani msikiti, kanisa na sinagogi.

Mchungaji Hohberg, Rabbi Tovia na Imamu Kadir Sanci ©Independent
Nyumba hiyo ya ibada itakayofahamika kama House of One, itakuwa na majengo matatu yenye maumbo tofauti, lakini yote yenye ujazo wa aina moja (idadi ya watu) ni wazo ambalo KWA TAARIFA YAKO limeanzia kutoka jumuiya ya Kikristo, tena kwa mchungaji, ambapo hadi sasa uwezeshwaji wa hali na mali ndio unaosubiriwa ili ijengwe.

Mchungaji Pfarrer Gregor Hohberg© House of One
Pamoja na hisia tofauti kuhusiana na nyumba hiyo ya ibada, Mchungaji Gregor Hohberg kutoka kanisa la Protestant anaeleza kuwa amefikiria hivyo na kuamua nyumba hiyo iwe jijini Berlin, mahala ambapo KWA TAARIFA YAKO lilikuwepo kanisa la kwanza liitwalo Mtakatifu Petro (St. Peter), ambalo lilikuwepo kwenye karne ya 12, kabla halijaharibiwa kwenye vita kuu ya pili ya dunia.

Mfano wa nyumba hiyo ya ibada itakavyokuwa
Pamoja na kuwa na mitazamo tofauti kuhusu ujenzi wa nyumba hii ya ibada, wengine wakiihuisha na siku za mwisho, KWA TAARIFA YAKO pande zote zinazohusika kiimani na jengo hilo zilishafahamishwa na kuonyesha kuunga mkono jambo hilo la kipekee ambalo halijawahi kuripotiwa kwenye tasnia ya dini ulimwenguni.
Rabbi Tovia Ben Chorin ©House of One
Miongoni mwa viongozi wa dini hizo walioshirikishwa ni pamoja na Rabbi Tovia Ben Chorin, kiongozi wa wayahudi, ambapo alisema kwamba wanaweza kuelewana vema tu, na kwamba anatambua ya kuwa kuna ambao hawatokubaliana nalo, na KWA TAARIFA YAKO akaongeza kuwa hilo si tatizo lao, na kwamba ni kila jambo lina mwanzo wake, na huo ndo wameuanza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni